Auawa akishangilia ushindi wa CHADEMA Kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa huko Shinyanga!

Imeelezwa kuwa uchaguzi wa kuwapata viongozi wa Serikali za Mitaa nchini uliofanyika juzi Jumapili umeendelea kumwaga damu ambapo mwanaume mmoja aliyefahamika kwa jina la Simeo Isaka (42), mkazi wa kijiji cha Ngokolo kata ya Bukomela wilayani Kahama mkoani Shinyanga, ameuawa kwa kukatwa na jembe kichwani na watu wasiojulikana wakati akishangilia ushindi wa mgombea wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) katika ngazi ya Uenyekiti wa Kijiji.
Tukio hilo limeripotiwa kutokea usiku wa kuamkia jana Jumatatu.
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga Justus Kamugisha ameripotiwa kuthibitisha kutokea kwa tukio hilo.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
No comments :
Post a Comment