tunakuchimbulia mpaka mwisho

LICHA YA USTAA ALIOPATA MAISHA ANAYOISHI BIBICHEKA YANASIKITISHA..!!

No comments
Hivi ndivyo unavyoweza kusema wakati unapomuona msanii wa muziki wa kizazi kipya, Cheka Hija, maarufu kama Bi. Cheka kutoka Kundi la Mkubwa na Wanawe, linaloongozwa na Said Fella ‘Mkubwa’ lenye maskani yake, Temeke jijini Dar es Salaam.
 
Bi Cheka akiwa nje ya nyumba anayoishi.


Mtoa habari wetu aliwasiliana na gazeti hili na kulieleza kuwa msanii huyo mwenye umri wa miaka 55, hivi karibuni alianguka ghafla nyumbani kwake na kukata kauli, wakati alipokuwa akienda chooni kujisaidia.
Wikiendi iliyopita, Amani lilifika nyumbani kwa msanii huyo mzee, anayeishi Bunju B, nje kidogo ya jiji la Dar na kumkuta akiwa na wajukuu zake huku hali yake ikiwa tete tokea alipoanguka Oktoba mwaka huu.
Akiwa anaishi katika kijumba chake kilichojengwa kwa miti na kukandikwa udongo, mtu anayemuona katika luninga akifanya vitu vyake, asingeweza kuamini kama hapo ndipo anapoishi.
 
Upande wa nyumba yake.
“Ukweli nilikuwa na hali mbaya, afadhali sasa, naongea na kusimama kwani nilikuwa siwezi kutembea, wiki iliyopita alikuja meneja wetu, Yusuf Chambuso na akina Dogo Aslay.
“Jamani maisha yangu kwa sasa ni magumu kwani siwezi kufanya kazi yoyote na sina msaada na kwenye muziki sijaona faida yoyote labda ya nguo tu, kwamba nilizoea kuvaa madela na kanzu sasa nina suruali,” alisema Bi Cheka kwa machungu.
 
Bi Cheka akiwa na wajukuu zake.
Alisema anasikitishwa na maisha yake kwani kutokana na umaarufu wake, mtaani kwao anaonekana kama mtu mwenye uwezo, wakati siyo kweli kwani anaishi kwenye nyumba ya tembe katikati ya nyumba nzuri.

“Kuhusu malipo makubwa kuwahi kupata ni shilingi laki tatu nilizolipwa kwenye shoo ya Fiesta mwaka juzi, hizo ndizo hela kubwa niliyowahi kupata katika muziki.”Gazeti hili lilimtafuta Fella ambaye alikiri Bi. Cheka kuumwa, akisema anasumbuliwa na magonjwa ya uzee na kwamba ahadi yake ya kumsaidia kujenga nyumba imeishia kwenye mchango wake wa matofari.

No comments :

Post a Comment